Showing posts with label ARUSHA NEWS. Show all posts
Showing posts with label ARUSHA NEWS. Show all posts

Tuesday, September 18, 2018

SHIRIKA LA WORLD VISION TANZANIA LAKABIDHI MRADI WA WORLD VISION -MUKULAT ADP WILAYANI ARUMERU MKOANI ARUSHA KWA WANANCHI NA SERIKALI BAADA YA KUUSIMAMIA KWA MIAKA 15

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha Dk. Charles Mahera mwenye shati la mikono mirefu akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la World Vision Tanzania mkoani Arusha pamoja na wawakilishi wa wananchi wilayani Arumeru mkoani hapa wakati wa kufunga Mradi wa World Vision -Mukulati ADP

Tuesday, August 7, 2018

SHIRIKA LA WORLD VISION TANZANIA, TAASISI YA AMARANTH NA ECHO WAKUTANISHA WATAALAMU MASUALA YA AFYA NA LISHE KWENYE KONGAMANO LA LISHE MAENEO KAME NCHINI




Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Richard Kwitega mwenye Tai akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa masuala ya afya na lishe bora kwa mama mjamzito na mtoto mara baada ya kufungua kongamano la Kimataifa kuhusu Lishe maeneo kame nchini  

Monday, August 6, 2018

WANANCHI WAVUTIWA BANDA LA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII VIWANJA VYA MAONYESHO YA NANE NANE NJIRO ARUSHA

 Afisa Mwandamizi wa Utalii Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro Gibson Olemtara akimsikiliza mmoja wa wananchi waliotembelea kwenye banda la Wizara ya Maliasili na Utalii Viwanja vya Maonyesho ya Nane Nane Njiro Arusha ambapo Mashirika yaliyopo chini ya Wizara hiyo yamepiga kambi kwenye banda hilo kwa ajili ya kukithi kiu za wananchi kuhusu utalii.

WAKULIMA WALIOTEMBELEA BANDA LA TAHA MAONYESHO YA NANE NANE NJIRO WAAHIDI MAKUBWA KWENYE MASHAMBA YAO

Baadhi ya wananchi wakiwa katika Banda la Asasi kilele ya sekta binafsi inayojishughulisha na kuendeleza tasnia ya horticulture nchini Tanzania (TAHA), kwenye Viwanja vya Maonyesho ya Nane Nane Njoro Arusha yanayojumuisha Mikoa ya Kanda ya Kaskazini.

TANESCO YAWAONYA WACHAKACHUAJI WA MITA MIAKA MITANO JELA ITAWAHUSU



Msimamizi wa Kitengo cha Mita Mkoa wa Arusha, Charles John.   




NA MWANDISHI WETU-ARUSHA

SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO), limewataka wananchi wa mikoa ya Kaskazini kujiepusha na vitendo vya kuchakachua Mita za umeme kwani atakayekutwa ametenda kosa hilo atafungwa jela miaka mitano.

Friday, July 13, 2018

WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEKEZAJI WA KAMPUNI YA MWIBA HOLDING


Mmoja wa Wakurugenzi Kampuni ya Mwiba Holdings, Abdukadir Mohammed akielezea mipango ya uwekezaji wa kampuni hiyo wilayani Meatu mbele ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa Manyara waliopotembelea  kampuni hiyo.



WANANCHI wa Mkoa wa Simiyu, Arusha, Mara, Shinyanga na Mwanza wametakiwa kuchangamkia fursa zinazotokana na uwekezaji unaofanywa na Kampuni ya Kitalii ya Mwiba Holding Ltd katika Pori la Akiba Maswa.

Mpaka sasa Taasisi ya Friedkin Conservation Fund (FCF), inayoendesha Kampuni za Mwiba Holding, Tanzania Game Trackers Safaris(TGTS) na Wingert  Safaris imewekeza zaidi ya Sh Bilioni 670 katika maeneo tofauti ya kitalii nchini.

Thursday, June 28, 2018

ASASI YA WATU NA WANYAMA (TPW), YAIWEZESHA BAWAKIMO SH MILIONI 40 ZA MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA NA UFUGAJI WA NYUKI

Msimamizi wa miradi wa Asasi ya Watu na Wanyama ya (TPW), iliyopo Simanjiro mkoani Manyara akizungumza wakati wa kukabidhi mradi mpya wa uhifadhi mazingira na ufugaji nyuki kwa Baraza la Wanawake wa Kikufugaji Monduli (BAWAKIMO), Asasi hiyo imewapa Sh milioni 40 kama mtaji kwa  wanawake 250 wa Kata ya Lemooti na Mswakini  wilayani Monduli.

Monday, June 4, 2018

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA WANYAMAPORI (TAWA), YAMWANGA MILIONI 50 UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA UFUNDI SIMIYU

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka akielezea kwa wanahabari faida na umuhimu wa Pori la Akiba la Maswa, lililowezesha kupitia mapato yanayokusanywa kupitia shughuli za utalii wa picha na uwindaji wa kitalii kuchangia mkoa huo Sh milioni 50 za ujenzi wa majengo ya Shule ya  maalumu ya vipaji ya Sekondari ya Ufundi Simiyu inayojengwa mjini Bariadi.Fedha hizo zilitolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini (TAWA)

Monday, April 30, 2018

TANAPA YACHANGIA MILIONI 50 UJENZI SEKONDARI YA UFUNDI SIMIYU



Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi akimkabidhi mfano wa Hundi ya Sh milioni 50, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka, kushoto ni Meneja Uhusiano wa TANAPA Paschal Shelutete na kulia mwisho ni Mkuu wa wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga. 

Monday, April 23, 2018

COMMERCIAL BANK OF AFRICA (CBA) TANZANIA, IPO IMARA NA SALAMA KWA ZAIDI YA ASILIMIA 100

Afisa Mtendaji Mkuu wa Commercial Bank of Africa (CBA) Tanzania, Gift Shoko akizungumza na wateja wa benki hiyo mkoani Arusha wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa kwa lengo la kuwashukuru kwa kuendelea kuwaamini, kuwaelezea maendeleo yanayotokea na kupokea mrejesho kutoka kwa wateja wao, halfa hiyo ilifanyika Mount Meru Hoteli mjini hapa. 

Sunday, April 15, 2018

MAONYESHO YA SEKTA YA UTALII YAJULIKANAYO KARIBU KILIFAIR KUFANYIKA JUNI 1 HADI 3, MWAKA HUU MJINI MOSHI

Wakurugenzi Watendaji wa KILIFAIR wa kwanza kulia Dominic Shoo na watano kutoka kulia Tom Kunkler, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wao wakati wa hafla ya kutambulisha maonyesho ya utalii yajulikanayo kama KARIBU KILIFAIR yatakayofanyika mjini Moshi Juni 1 mpaka 3, mwaka huu. Hatua hiyo imekuja baada ya kuungana kwa KARIBU FAIR na KILIFAIR.

Tuesday, April 10, 2018

JENGO la kitega uchumi la Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro jijini Arusha ambalo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika mwezi juni mwaka huu litakuwa kivutio cha kihistoria cha utoaji wa huduma za utalii hapa nchini.


Na Hamza Temba - WMU
........................................................
JENGO la kitega uchumi la Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro jijini Arusha ambalo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika mwezi juni mwaka huu litakuwa kivutio cha kihistoria cha utoaji wa huduma za utalii hapa nchini.

NDEGE VIVUTIO VINAVYOCHANGIA KUIMARISHA MAPATO KWENYE SEKTA YA UTALII NCHINI



JAMII nchini imetakiwa kuwatunza na kuwalinda ndege waliopo kutokana na kuwa sehemu ya vivutio vinavyochangia kuimarisha mapato kwenye sekta ya utalii.

ASASI YA NATURE TANZANIA YAHAMASISHA KUTUNZA NDEGE KWA AJILI YA UTALII


Baadhi ya wafanyakazi, watafiti wa masuala ya uhifadhi na utalii na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Nature Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mjini Arusha 

Monday, April 9, 2018

RC GAMBO AAGIZA KILA HALMASHAURI ARUSHA IPANDE MITI MILIONI 1.5 KWA MWAKA



Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo ameziagiza halmashauri zote za mkoani humo  kupanda miti milioni 1.5 kwa mwaka ili kutunza mazingira.

Thursday, March 29, 2018

KLABU ZA BIASHARA MWAROBAINI WA TATIZO LA AJIRA TANZANIA YA VIWANDA


 Mkurugenzi wa Shule ya Ester Memorial Academy

-ARUSHA
ELIMU ya ujasiriamali kupitia Klabu za Biashara inayolenga wanafunzi wa Shule za Msingi,Sekondari na Vyuo kujifunza kwa vitendo, kuweka akiba na kupata kipato imetajwa kuwa ni mwarobaini wa tatizo la ajira nchini.

Wednesday, March 21, 2018

TANZANIA NA UJERUMANI ZAKUBALIANA KUENDELEZA TAFITI ZA MASALIA YA MIJUSI KATIKA ENEO LA TENDAGURU MKOANI LINDI


Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Maj. Gen. Gaudence S. Milanzi (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Historia Asilia ya Berlin Ujerumani (Berlin Museum of Natural History), Prof. Johannes Vogel kuhusu masalia ya mjusi wa Tanzania yaliyofadhiwa katika makumbusho hiyo.