Friday, June 9, 2017

KESI MMILIKI LUCKY VINCENT YAPIGWA KALENDA

Na JANETH MUSHI,
-ARUSHA

MAHAKAMA ya wilaya ya Arusha imeahirisha kesi inayomkabili mmiliki wa Shule ya Lucky Vincent  Innocent Mushi, hadi Julai 5,Mwaka huu kutokana na upelelezi kutokukamilika.


Mtuhumiwa huyo pamoja na mwenzake ambaye ni Mwalimu Mkuu Msaidizi Longino Nkana waliounguliwa kesi na 78 ya Mwaka huu wanatuhumiwa kwa makosa ya usalama barabarani ikiwamo kusafirisha watoto bila kuwa na vibali muhimu.

Mushi aliburuzwa kwa mara ya kwanza  Mei 12,Mwaka huu  katika  Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha,ambapo anakabiliwa na  mashitaka manne ya usalama barabarani.

Mbele ya Hakimu Desderi Kamugisha,Wakili wa Serikali Alice Mtenga,aliiomba mahakama hiyo kuahirisha kesi hiyo na kuipangia tarehe nyingine kutokana na upelelezi wa kesi hiyo kutokukamilika.

Watuhumiwa hao walikuwa wakitetewa na Wakili Method Kimomogoro ambapo Hakimu Kamugisha alikubaliana na wakili huyo na kuahirisha kesi hiyo hadi Julai 7,Mwaka huu.

Awali wakisomewa mashitaka yao Mei 12,Mwaka huu, Wakili wa Serikali Rose Sule alidai mtuhumiwa wa kwanza Mushi anakabiliwa na makosa manne wakati Nkana akituhumiwa kwa kosa moja.

Wakili Sule alidai kwamba Mushi akiwa Mkurugenzi wa Shule ya Lucky Vicent anatuhumiwa kuendesha gari la abiria bila ya kuwa na Leseni ya usafirishaji.

Alidai kuwa Mei 6, Mwaka huu katika eneo la Kwamrombo wilayani Arusha mtuhumiwa huyo alifanya shughuli ya usafirishaji wa abiria akiwa ana mmiliki gari aina ya Mitsubish Rossa T. 871 BYS. 

Aliendelea kudai mahakamani hapo kuwa kosa la pili linamkabili mtuhumiwa huyo ni la kuruhusu kuendeshwa kwa gari bila kuwa na Bima (Road Licence), ambapo Mei 6, Mwaka huu aliruhusu gari hilo kuendeshwa huku akijua halina Bima.

"Kosa la tatu ni kushindwa kuingia mkataba na mwajiri wake ambapo Mei 6, Mwaka huu ukiwa mmiliki  wa gari hilo ulishindwa kuingia mkataba wa ajira na dereva wako Dismas Joseph Gasper ambaye kwa sasa ni marehemu,” alidai Wakili Sule alipokuwa akisoma mashitaka na kuongeza:

"Mtuhumiwa unakabiliwa na kosa la Nne ambalo ni la kubeba abiria waliozidi zaidi ya 13 ambapo Mei 6, Mwaka huu ukiwa Mkurugenzi, Afisa Msafirishaji na mmiliki wa Lucky Vicent ulibeba na kusafirisha abiria zaidi ya 13, kinyume cha sheria,” alidai.

 Wakili Sule akisoma mashitaka kwa mtuhumiwa wa pili alidai mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa Nkana anadaiwa kukandaa safari iliyozidi abiria 13 huku akijua ni kinyume cha sheria.

 Alidai kuwa Mei 6,Mwaka huu mtuhumiwa huyo akiwa na nafasi ya Mwalimu Mkuu Msaidizi  na mwandaaaji wa safari hiyo aliruhusu kupakia abiria zaidi ya 13 kwenye gari liliosababisha vifo vya watu.
  

Mwisho.

No comments:

Post a Comment