Na
MWANDISHI WETU
-ARUSHA
SHIRIKA
la Maendeleo ya mitaji la umoja wa Mataifa (UNCDF) imewajengea
uwezo Manispaa na Majiji matano nchini, ili waweze kupanua wigo wa uwekezaji kwa ajili ya kuboresha maeneo
yao na kukopesheka katika soko la
hisa.
Akizungumza
jana Jijini hapa Mkuu wa shirika la Maendeleo ya Mitaji la
Umoja wa mataifa (UNCDF), Peter Malika alisema wameamua kuendesha
warsha ya kimataifa ya siku mbili kwa
kushirikiana na Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa ili Manispaa na Majiji hayo yanufaike na masoko
ya mitaji Tanzania kwa kuwekeza katika soko la
hisa kwa kuuza vipande na kuutoa
hati za dhamana.
Alisema
ni vizurimajiji na manispaa wakabaini njia nzuri za kutafiti miradi
ya maendeleo ya kiuchumi na utoaji huduma hatimaye waboreshe maisha ya wananchi wao na kukuza vipato vya majiji na
halmashauri zao.
“Majiji
tuliokutanisha ni Mwanza,Arusha,Mbeya,Tanga na Dar es Salaam,pamoja
na manipsaa tatu za Kinondoni,Temeke, Ilemela na Dodoma zenye uwezo wa kuanza kuwekeza katika soko la hisa kwa
kuuza hati za
dhamana za manispaa,”alisema.
dhamana za manispaa,”alisema.
Alisema
UNCDF ipo katika nchi 48 Duniani kazi yake kubwa inafungua rasilimali
za umma na binafsi hasa ngazi za nyumbani ili kupunguza umaskini na kusaidia maendeleo ya kiuchumi.
Naye
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho gambo akifungua warsha hiyo kwa niaba
ya Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa, George Simbachawene, aliipongeza UNCDF na
Mamlaka za serikali za mitaa kwa juhudi za kutafiti njia mbadala
zinazoweza kutumiwa na mamlaka za serikali
za mitaa kuongeza mapato kwa ajili ya uwekezaji miradi ya maendeleo ya uchumi.
Alisema
kutokana na mahitaji mengi ya malamlaka za serikali za mitaa yasioendana
na fedha kinahitajika kuzisaidia mamlaka ya serikali za mitaa,majiji na manispaa kuwa na njia mbadala za
kuongeza mapato yatakayowezesha
kugharamia majiji yanayokua kwa kasi kubwa.
Gambo
alisema anatumaini baada ya warsha hiyo wajumbe wataweza kutoka na
mikakati ya kifedha itakayopima faida na hasara ya kutoa hati za dhamana za manispaa katika mazingira ya Tanzania kwa
kuchambua mahitaji,vigezo na
masharti katika maandalizi ya uwekezaji.
Alisema
UNCDF itawezesha manispaa na majiji kukabiliana na changamoto za
kifedha kwa kuimarisha huduma za msingi za ndani,kukuza maendeleo
ya uchumi nma kuongeza uthabiti wa ndani na hali
ya hewa na majanga ya
kiuchumi.
kiuchumi.
“Mbinu
inatambua kuwa uchumi wa taifa umeongezeka kwa kasi zaidi kwa muda
wa muongo mmojauliopita hata hivyo uwekezaji duni katika ngazi za
chini bado ni kikwazo kikubwa katika mabadiliko
ya miundombinu ndani
ya manispaa,”alisema.
ya manispaa,”alisema.
Mkurugenzi
wa Jiji la Arusha Athuman Kihamia, alisema wamekutana majiji
matano Tanzania Bara na masispaa tatu, wanaongelea mambo ya uwekezaji na majiji haya yanatakiwa kwenda
jkisasa zaidi tofauti na zamani.
Wanajadili
namna bora ya kuwekeza ili waweze kukopa na kuendesha miradi
mikubwa kwa ajili ya kuingia soko la hisa kama kampuni binafsi
na umma.
Mwisho
No comments:
Post a Comment