NA JACKLINE LAIZER
-ARUSHA
MWANARIADHA Gabriel Geay wa Tanzania amelamba kitika cha
Dola 8000 baada ya kufanikiwa kushika nafasi ya kwanza katika mashindano ya
mbio za Km 10 za Bolder Boulder zilizofanyika juzi nchini marekani.
Geay alifanikiwa kuchukuwa kitika hicho baada ya kutumia
muda wa dakika 29:02:19, huku mshindi wa pili ni Leonard Korir wa nchini
Marekani yeye alitumia dakika 29:02:81 na mshindi wa tatu ni Sam Chelanga nae
wa nchini Marekani alitumia dakika 29:07:66.
Akizungumza mjini hapa Katibu wa Shirikisho la Riadha Tanzania
(RT) Wilhelm Gidabuday alisema wanariadha watatu ndiyo walikwenda kuwakilisha
nchi katika mashindano.
Aloiwataja wanariadha wengine kuwa ni Ismail Juma aliyeshika nafasi ya
18 na Josephat Gisemo aliyemaliza katika nafasi ya 20, huku katika matokeo ya
jumla Tanzania imeshika nafasi ya nne.
"Nawashukuru wanariadha wote wanaofanya vizuri katika
mashindano mbalimbali kwani fursa tunazowatafutia wamekuwa wakuzitumia vizuri
kwa kupata ushindi, ila ninatoa onyo kali kwa mwanariadha yeyote ambae
chama kinamtafutia mashindano halafu anakataa kwenda kushiriki kwani huo ni
utovu wa nidhamu na hautakubalika" alisema Gidabuday.
Alisema mwanariadha yeyote ajira yake ni mbio na
muda wowote lazima awe tayari katika mashindano yatakayoweza kujitokeza mbele
hivyo ni nini sababu ya mwanariadha kukataa kushiriki mashindano ambayo
umetafutiwa tena kwa faida yake.
Gidabuday aliongeza bado wataendelea kuwatafutia
wanariadha wao mashindano ya kutafuta viwango vya kushiriki mashindano ya Dunia
yatakayofanyika Agost mwaka huu nchini Uingereza.
"Mashindano ya mbio zozote za kutafuta viwango ni ya
uwanjani isipokuwa viwango vya mbio za marathoni, na haya mashindano ya Bolder
Boulder yalikuwa ni ya barabarani hivyo ninawahaidi wachezaji kuwa bado tuna
muda wa kuwatafutia mashindano mengine kwa ajili ya viwango" aliongeza
Gidabuday.
Mwisho
No comments:
Post a Comment