Monday, January 8, 2018

WAZIRI SULEIMAN JAFO AKEMEA UTATU USIO MTAKATIFU MANUNUZI YA KAZI YA TARURA

NteghenjwaHosseah,Mbeya

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo amewataka watumishi wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijiji (Tarura) kuvunja utatu usio mtakatifu katika kazi za ujenzi na matengenezo ya barabara zinazoendelea kutangazwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo

   
Ameyasema hayo wakati wa kufungua mafunzo ya siku Sita ya watalaam wa Tarura kutoka katika Mikoa saba ya Nyanda za Juu Kusini kuhusiana na masuala ya Ununuzi wa Umma na Usimamizi wa Mikataba ya Ujenzi na matengenezo ya barabara na Maadili katika kazi za TARURA yenye takribani miezi Sita tangu kuanzishwa kwake.

Waziri Jafo amesema "Ninaposema Utatu mtakatifu namaanisha Afisa Manunuzi, Mhasibu na Mhandisi wa Tarura katika eneo husika hawa ndio huwa wanaamua nani apewe kandarasi kwa mujibu wa mahusiano na makubaliano wanayoyajua wao."

Huu Utatu usio mtakatifu katika kazi za Umma ufe kuanzia leo na Mkandarasi apewe kazi kwa kuzingatia uwezo wake wa kitaalam na kifedha katika kukamilisha kazi hiyo nasio mahusiano na makubaliano nje ya vigezo vilivyowekwa".

Katika Utatu huu ninauo uzungumzia kuna mahusiano ya karibu sana na rushwa na ina fahamika wazi kuwa rushwa hupofusha wataaalam kuona na kutathmini uwezo wa Mzabuni, huzorotesha kazi iliyopangwa kufanyika na kuwanyima wananchi haki yao ya msingi ya huduma bora za barabara na tutakaowabaini wakiendeleza kasumba hii tutawachukulia hatua za kisheria na kinidhamu alisema Jafo.

Akimkaribisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala amesema wamejiandaa kikamilifu kusimamia kazi za Tarura na baada ya uzinduzi wa kitaifa walizindua tena Kimkoa ili kuwafahamisha wananchi wa mkoa huo umuhimu wa Taasisi hii, ili waweze kumiliki kazi zinazofanywa na Tarura na kuwaelewesha lengo la kutoka kazi za barabara kutoka Halmashauri na kusimamiwa na Tarura.

   Waziri Jafo (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala 

“Tarura imekuja kuboresha kazi nzuri iliyokuwa ikifanywa na Baraza la madiwani, Kamati za kudumu pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi sasa TARURA wamekuja kutekeleza kitaalam zaidi, namna ya usimamizi, manunuzi, mikataba ili tuweze kupata matokea bora na ya haraka.

Naye Mkurugenzi wa Tarura Eng. Abdul R. Digaga amesema mafunzo haya ni mpango wa kimkakati wa  Tarura katika kupambana na rushwa katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi na matengenezo ya barabara,mgongano wa maslahi, matumizi mabaya  ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara na ukosefu wa uadilifu miongoni mwa watendaji. 

Waziri Jafo (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Barabara Vijijini Mhandisi Abdul Digagab 

Mafunzo hayo ambayo yalianza kufanyika katika kanda mbalimbali nchini na kanda hii ya Nyanda za juu kusini ni ya mwisho kufanyika kwa wataalam wa Tarura wa kada mbalimbali na imejumuisha Mikoa ya Mbeya, Songwe, Ruvuma, Rukwa, Katavi na Iringa na Njombe.


 Baadhi ya wataalamu wa TARURA wa kifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, OR-TAMISEMI Selemani Jafo wakati akifungua mafunzo ya Manunuzi na Maadili Jijini Mbeya
Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Selemani Jafo(aliyekaa katikati) na viongozi wa Mkoapamoja na TARURA na washiriki wa mafunzo kutoka Mkoa wa Njombe.



No comments:

Post a Comment