Wednesday, January 3, 2018

SIHA WAPATA NEEMA UKAMILISHWAJI HOSPITALI YA WILAYA

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo akisaini kitabu cha wageni wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya wilaya ya Siha, pembeni yake ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira


Na Nteghenjwa Hosseah, Siha.

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo amesema atafanya kila liwezekanalo kupata fedha zaidi kwa ajili ya ukamilishaji wa hospital ya wilaya ya Siha.


Waziri Jafo amesema hayo alipokuwa akifuatilia agizo lake alilolitoa miezi kadhaa iliyopita ya kuacha kutumia Mkandarasi na kutumia mafundi wa jamii "Force Account" katika ujenzi wa hospital hiyo ambapo Halmashauri ya Siha ilishatoa kazi hiyo kwa Mkandarasi na gharama za ujenzi kuwa juu zaidi.


"Katika ziara yangu iliyopita kazi ilikuwa haijaanza na bado mlikuwa mnajadiliana na Mkandarasi mlinieleza kuwa zinahitajika fedha zaidi kwa ajili ya kukamilisha kazi hii kwa mujibu wa Mkandarasi ndipo niliposhauri mtumie mafundi wa kijamii "Force Account" nasi mkandarasi kama mlivyopanga hapo awali," alisema Waziri Jafo.


  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo (katikati) akikagua ukamilishaji wa  Hospital ya wilaya ya Hai alipofanya ziara yake katika wilaya hiyo.

   Hili ni kati ya majengo ya nayoendelea kujengwa katika  Hospitali ya wilaya ya Hai.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo akizungumza na watumishi wa Idara ya Afya wakati alipotembelea Hospital ya wilaya ya Hai.

Aliongeza "nimefurahi kuwa mlinielewa na mkazingatia ushauri wangu na leo hii ninaona matunda ya matumizi ya mafundi wa kijamii ambao wamefanya  kazi nzuri kwa ubora wa hali ya juu na gharama nafuu katika hili hongereni sana".

Alisisitiza kuwa nimeona majengo ambayo yanakaribia kukamilika lakini pia nimeskia taarifa yenu kuwa bado kuna majengo zaidi ya nahitajika ila kukamilisha hadhi ya hospital ya wilaya nina ahidi kuwa tafutia fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo hayo.

Akisoma taara ya Afya Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Dk. Andrew Method amesema wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa Hospital ya wilaya na vituo vya Afya vilivyopo ni vitano tu ambavyo kati ya hivyo cha Serikali ni kimoja tu hivyo nguvu kubwa imewekwa katika kuhakikisha wanapata miundombinu bora ya hospital ya wilaya.

"Fedha tulizopata ilikuwa ni Sh milioni 200 na kwa kuzingatia maelekezo yako tulitumia Force Account na kama unavyoona kazi iko katika hatua za mwishoni, ".

Ujenzi wa Hospital hii utakapo kamilika utawezesha wilaya ya Siha kuwa na hospital moja ya wilaya pamoja na ile ya Kibong'oto iliyoko chini ya Wizara ya Afya.


 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro, pamoja na watumishi wa Halmashauri hiyo.


No comments:

Post a Comment