Na MWANDISHI WETU
-ARUSHA
WADAU wa Utalii mkoani Arusha wamekutana kujadili mikakati ya kuipaisha sekta hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi.
Majadiliano hayo
yalifanyika mjini Arusha juzi, na kuhudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho
Gambo, Chama cha Wafanyabiashara wa Utalii (TATO) na Shirika la Hifadhi za
Taifa nchini (TANAPA).
Akizungumza katika
warsha hiyo Gambo alisema mkoa wa Arusha umekuwa ukichangia mapato ya utalii
nchini kwa zaidi ya asilimia 80. Hivyo kuna kila sababu ya kuboresha sekta hiyo
ili iendelee kuleta matokeo chanya kwa taifa.
Gambo katika
mkutano huo aliwataka wadau hao kushirikiana na viongozi wa mkoa kuandaa
tamasha kubwa la utalii la kimataifa litakalotumika kama jukwaa la kuutangaza
mkoa na taifa.
Kwa upande wake Mkurugenzi
Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi akizungumzia kuhusu tozo kuwa kubwa alisema bado
kuna muda wa kuendelea kujadili jambo hilo.
“Tunaamini awamu ya
tano ni sikivu, ni vyema tukipanga muda sisi wadau tujadiliane tuone namna ya
kuishauri Wizara,” alisema Kijazi.
Aidha, TATO katika
mkutano huo waliainisha changamoto wanazokutana nazo katika biashara hiyo.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment