Friday, June 2, 2017

MWANGAZA VETERANI KUKIPIGA VS KITAMBI NOMA

Na  JACKLINE LAIZER

-ARUSHA

TIMU ya Mwangaza Veterani inatarajiwa kushuka dimbani kesho (Jumapili) kupambana na Kitambi Noma katika mchezo wa kirafiki utakaochezwa katika uwanja wa Kitek uliopo Suye nje kidogo ya jiji la Arusha.


Akizungumza mjini hapa jana Katibu mkuu wa Timu ya Mwangaza Veterani Charles Swati alisema maandalizi kuelekea mchezo huo wa kirafiki na mahasimu wao umekamilika, na wachezaji wake wapo katika mazoezi mepesi kujiandaa na mtanange huo.

“Katika kuhakikisha tunatekeleza agizo la Makamu wa Rais mama Samia Suluhu kuwa inatupasa kufanya mazoezi ili kuimalisha miili yetu tumeamua kuandaa mchezo huu wa kirafiki ukiwa na lengo la kuhamasisha kila mtu anahitajika kufanya mazoezi kwa faida yake" alisema Swati.

Alisema lengo lingine la kucheza mchezo huo wa kirafiki ni katika kuhakikisha wanadumisha mahusiano na urafiki mwema kati ya mfanyakazi na mfanyakazi kwani wakishirikiana kwa pamoja upendo na ufanisi wa kazi utazidi mara dufu.

Alisema miili inayojiimalisha na mazoezi inakuwa imara zaidi ya ile ambayo haijihusishi na mazoezi na wanatumia michezo kuendelea kupiga vita utumiaji wa madawa ya kulevya.
“Tumeamua kuwaalika timu ya Kitambi noma kwa kuwa ni maveteran wenzetu ambao na pia tumekuwa na upinzani nao mkubwa katika michezo hivyo mchezo huo utakuwa na hisia ya aina yake”alisema Swati.

Aidha alieleza kuwa mara baada ya mpambano huo timu ya Mwangaza Veterani inajiandaa kwenda Babati kuchuana vikali na timu  ya Babati Veterani  hivi karibuni.

Timu ya Mwangaza Veteran ninaundwa na wachezaji walicheza soka miaka ya nyuma wakiwa na lengo la kuwajenga na kuwanyanyua vijana wanaochipukia katika soka na hivi karibuni Mwangaza veteran ilishuka dimbani kucheza na timu ya AICC veteran mchezo uliomalizika kwa kushinda mabao 4-2.


Mwisho

No comments:

Post a Comment