Na ELIYA MBONEA
-ARUSHA
KAMPUNI ya Tanzanite One na Shirika la Madini nchini (STAMICO),
wanaochimba madini ya Vito ya Tanzanite wametakiwa kutowarudisha nyuma zaidi,
wachimbaji wadogo pindi wanapotoboza eneo la Delta linalomikiwa kisheria na
mwekezaji huyo.
Wito huo ulitolewa mjini hapa juzi na Kamishna Msaidizi wa
Madini Kanda ya Kaskazini Adam Juma alipozungumza na MTANZANIA kuhusu usalama
migodini, uzingatiaji mipaka, sheria na umuhimu wa ramani ya uchimbaji (mining
plan).
Kauli hiyo ameitoa huku tayari baadhi ya wachimbaji wadogo
wakiripotiwa kupigwa mabomu ya machozi chini ya ardhi, kunyang’anywa vifaa vya
kazi na Wakaguzi wa mwekezaji wanaoshirikiana na askari polisi waliopo kituo
cha mgodini.
Akifafanua mitobozano ya wachimbaji wadogo waliopo Kitalu D
dhidi ya Mwekezaji aliyepo Kitalu C, Juma alisema tangu Mei mpaka Juni,
Mwaka huu kumekuwa na muingiliano mkubwa kutokana Tanzanite One kuanza
uzalishaji katika eneo la Delta.
“Wachimbaji wadogo wanachimba eneo la Delta kwasababu hakuna
kikwazo chochote kwa vile muhusika wa eneo hilo kisheria alikuwa halichimbi.
Lakini sasa ameanza kufanya uzalishaji kwenye eneo hilo,” alisema Juma na
kuongeza:
“Tunasisitiza kwa Tanzanite One wasiwanyang’anye kabisa maeneo
au kuwarudisha nyuma zaidi kunapotokea mtobozano, kwasababu bado taarifa ya
Kamishna wa Madini kupitia Kamati ya kuangalia upya ramani zote mgodi hapo
haijatoka,” alisema.
Akitoa mifano ya mitobozano ya hivi karibuni kwa wachimbaji
wadogo wa Kitalu D, Kamishna Msaidizi Juma alisisitiza majadiliano yanayolenga
kuimarisha usalama migodini hususani kwa wakaguzi wa mwekezaji.
“Shafti ya Delta inayoongelewa ipo mpakani na Kitalu D kama Mita
100 kutoka mpaka wa Kitalu C.Tunasisitizamajadiliano zaidi mfano mwekezaji
akikuta umetoboza mpaka kwake anaweza kukurudisha nyuma zaidi Mita 20 kwa
usalama ambayo bado ni kumpa upendeleo mchimbaji mdogo,” alisema Juma.
Alisema kutokana na sheria kutoa maelekezo kwa kila mchimbaji
kufuata mipaka yake, aliwataka wachimbaji wadogo kuondoa dhana kuwa chini ya
ardhi hakuna mipaka ya uchimbaji huku akiwasisitizia wabadili muelekeo na fikra
za uchimbaji kuelekea Kitalu C ikiwamo kuwa na ramani ya uchimbaji (mining
plan).
Alisema Mei Mwaka huu, kupitia kikosi kazi walipima migodi yote
inayozunguka Kitalu C, yaani kitalu C na B ili wapate ramani ya pamoja
itakayowezesha kuangalia hali ya muingiliano.
“Ripoti imekabidhiwa kwa Kamishna wa Madini na Mkaguzi Mkuu wa
migodi, tunasubiria uamuzi. Tulichokiona ni muingiliano mkubwa kwani wengine
wamechimba mita 200 lakini wametoka nje ya eneo lao mpaka Mita 1,000 kuelekea
KIA,” alisema Juma.
Kwa upande wake mmliki wa mgodi namba 0000049 uliopo Kitalu D,
Theresia Wapalila alisema,wafanyakaz wa mgodi wake walivamiwa na watu wenye
silaha za moto kisha kuwapiga na kuwanyang’anya vifaa vya kazi.
“Watu hawa walivunja grill inayotenganisha mgodi wetu kupitia
bomba ambalo hatujui nani aliliweka,” alisema Wapalila.
Aidha taarifa ya ukaguzi uliofanywa na wajumbe wa kamati ya
usuluhishi ilibaini kuwa mgogoro huo ulitokana na kukusudiwa na wafanyakazi wa
Tanzanite One waliochungulia uelekeo wa mgodi a Wapalila.
Naye Mkurugenzi Mwenza wa Kampuni ya Tanzanite One Faisal Juma
akizungumzia malalamiko hayo alikiri kuwapo kwa malumbano.
Makubwa maeneo ya machimbo hususani wachimbaji wadogo ambao kwa
asilimia kubwa wameshindwa kutambua mipaka na kuheshimu sheria.
“Mgodi wa Tanzanite One si wa kwetu peke yetu pale
tunachimba kwa ubia na Serikali kupitia STAMICO.Hivyo ni lazima kuwepo na
usimamiaji makini wa kulinda mipaka na kuhakikisha maslahi ya umma yanalindwa,”
alisema Juma na kuongeza:
Eneo la Delta lipo kwenye lesesni ya Kitalu C kinachomilikiwa
kisheria na kampuni. Ni kweli wachimbaji wadogo katika harakati za kuchimba
wanapitiliza na kuingia eneo hilo. Sisi na serikali kwa pamoja tunayo haki ya
msingi kusimamia maeneo hayo.
“Hakuna namna mchimbaji anaweza kuepuka usalama mgodini ndio
maana kila mchimaji lazima awe na ‘mining plan’ yake,” alisema.
Mwisho.

No comments:
Post a Comment