Na ELIYA MBONEA
-BABATI
HOSPITAL
ya Dareda inayohudumia wagonjwa zaidi ya 150 kwa siku kutoka maeneo ya
Halmashauri ya wilaya ya Babati vijijini, mkoani Manyara haina mashine
ya kuzuia damu wakati wa upasuaji.
Aidha,
hospitali hiyo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mbulu,
ikiendeshwa kwa ubia na Serikali inakabiliwa pia na upungufu wa
vyandarua, mablanketi na mashine ya Ultra Sound.
Changamoto
hizo zilibainishwa juzi hospitalini hapo wakati wa hafla ya kukabidhi
msaada wa mashuka yaliyotolewa na Mfuko wa Mafao ya Kustaafu wa (GEPF)
na Mwenyekiti wa Bodi Joyce Shaidi.
Akizungumzia
changamoto hizo Mganga Mfawidhi Dk.Abraham Laizer alisema,hospitali
hiyo yenye vitanda 200 vya kuandikishwa kwa sasa ikabiliwa na ongezeko
kubwa la wagonjwa.
“Tuna
mahitaji makubwa ya vifaa ambavyo kama tungevipata nahakika juhudi zetu
za kusaidia na kuokoa maisha ya wananchi zingefanikiwa zaidi,” alisema
Dk. Laizer na kuongeza:
“Mahitaji
yetu sana ni mashine ya kuzuia damu wakati wa upasuaji na Ultra Sound.
Kwa msaada huu wa msahuka hakika tunawashukuru hasa ukiwa umeelekezwa
kwa mama na watoto,” alisema.
Alisema hospitali hiyo inapokea wagonjwa wa nje na wakulazwa ambapo wazazi wengi wamekuwa wakitumia kama kimbilio lao.
Alisema
kutokana na mazingira ya baridi yaliyopo kwenye eneo hilo jamii hasa
watoto wamekuwa wakikabiliwa na magonjwa ya Nimonia, magonjwa ya njia ya
hewa pamoja na majeraha kwa watu wa pikipiki na wakulima.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya GEPF Shaidi alisema, mashuka 100
wameyatoa kwenye hospitali hiyo kama sehemu ya kurudisha faida kidogo
kwa jamii.
“Tukiwa
Mfuko wa Pensheni huwa tunatoa mafao kwa ajili ya uzazi na kusaidia
huduma kwa mama baada ya kujifungua, tuliona hapa mna upungufu wa
mashuka kwa mama wajawazito baada ya kujifungua na watoto,” alisema
Shaidi.
Naye
Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Padri Peter Salahoo, alisema hospitali
hiyo ilianzishwa Mwaka 1947 na Shirika la Masista kisha kukabidhiwa kwa
Askofu wa Jimbo la Mbulu.
“Tupo
hapa kushirikiana na Serikali kuisaidia jamii tunatoa huduma mbalimbali
ikiwamo matibabu bila malipo kwa mama na mtoto chini ya miaka mitano
pamoja na wazee zaidi ya miaka 60.
“Eneo
hili ni la baridi kwa ujumla mahitaji bado ni mengi hasa kwa upande wa
mashine kama Ultra Sound ambazo huwasaidia madaktari kutambua mahitaji
ya kina mama pamoja na kuangalia mtoto anaendeleaje tumboni,” alisema
Padri Salhoo na kuongeza:
“Tunashukuru msaada huu wa GEPF lakini tunawaomba na wadau wengine watupie macho maeneo haya ya hospitali za vijijini,” alisema.
Katika
hatua nyingine hospitali hapo mara baada ya kutembelea na kujionea
mahitaji mengine naye Dk.Joseph Roli aliushukuru mfuko huo kwa msaada wa
mashuka kutokana na kukabiliwa na upungufu wa shuka za kutandika
vitandani.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment